Ballon d'or kurejea mwezi Novemba
Tuzo la mchezaji bora Wa dunia kurejea mwaka huu baada ya kutupiliwa mbali mwaka uliopita kwa Mara ya kwanza tangu kuanza kwake miaka 64. Hafla hii imeratibiwa kufanyika tarehe 29 mwezi Novemba.
Nyota Wa zamani Wa Chelsea na timu ya taifa Ivory Coast Didier Drogba na mwanahabari Wa michezo Sandy Heribert wanatarajiwa kuongoza sherehe hio.DROGBA NA SANDY.picha Hisani :Jpeg images.
MSHINDI
Tuzo la Balloon d'or kwa sasa mshikilizi ni nyota Wa kimataifa Wa Argentina Lionel Messi,akitarajiwa kuleta ushindani tena baada ya kuhamia Paris saint Germain ya ufaransa.Messi ameshinda Mara sita akifuatwa na Christiano Ronaldo Wa Manchester united.
USHINDANI.
Wengine waliorodheshwa katika kolamu ya ushindani mwaka huu ni mshambulizi Wa Bayern Munich Robert lewandwoski na kiungo kati Wa Chelsea Jorghino. Orodha rasmi kutolewa octoba 8.
Maoni
Chapisha Maoni