Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Septemba, 2021

kwanini Greenwood amekosekana kwenye kikosi cha South gate?

Picha
23 waitwa kikosini Uingereza . Beki kati Wa Acmilan Fikayo Tomori ameitwa katika kikosi cha timu ya taifa soka Uingereza maarufu Three lions kuziba pengo la Jacob Harry Maquire ambaye ni majeruhi.Mason Greenwood vilevile amekosekana katika kikosi hicho kitakachojiandaa kupagusana na Andorra na Hungary katika mechi za kufuzu dimba la Dunia mwaka 2022,Qatar. WALIOKOSA . Alexander-Arnold -  Arnold alicheza mechi ya septemba dhidi ya Andorra na anatarajiwa kukosa mechi ya  Liverpool dhidi ya  Manchester Cit y Jumapili ya kwanza octoba,pambano la ligi kuu Uingereza,kwa kuwa na jeraha. Greenwood Bamdogo mwenye kumiliki miaka 19, amekosa kikosi baada ya mabosi wa united kusema ni kazi nyingi kwa kinda huyu. Hatua kama hiyo,imeafikiwa na mabosi Wa Borrusia Dortmund kuhusu Jude Bellingham. Mlinda lango wa Burnley Nick Pope . Kuitwa kwa askari mango Wa Arsenal Aaron Ramsdel alisafiri na kikosi kilichofika fainali ya  Euro 2020,kumemnyima nafasi pope. Kikosi Nahodha wa spurs Harry Kane,Jack Grea

"Hatucheki kabla mechi........." muller atoa siri za Bayern kushinda

Picha
Mshambulizi matata wa Bayern Munich,Mjerumani Thomas Muller lisema "hatucheki na mpinzani kabla mechi,tunacheka ikikamilika ,ila uenda matokeo yakawa magumu kwake akakosa kucheka". Muller akizungumza baada ya mechi dhidi ya Dynamo Kiev mtanange Wa klabu bingwa. wachezaji Wa Bayern Munich katika uwanja Wa Allianz Arena. Picha: Getty images.

Afungwa wiki 8 kwa kumbagua kirangi mchezaji Wa westbrom .

Picha
Simon silwood ambaye ni shabiki kindakindaki Wa timu ya Westbromwhich Albion alifungwa jela wiki 8 tarehe 30 mwezi septemba,kwa kosa la ubaguzi Wa ranging dhidi ya mchezaji Wa westbrom Romaine Sawyer. Silwood ameshtakiwa kwa kosa la kuchapisha posti katika mtandao Wa Facebook akisema Sawyer anafaa kusbinda tuzo la Baboon D'OR badala ya Balloon d'or. Mawakili Wa Sawyer wamesema chapisho hilo lilivuruga amani na kuchangia ukosefu Wa utulivu kwa mteja wao.Romain kwa sasa anakipiga na stoke city kwa mkopo. picha za Romaine Sawyer. Picha: jpeg  MARUFUKU KUHUDHURIA MECHI . Timu ya Westbrom imempiga marufuku kuhudhuria Mechi zao Silwood mwenye umri Wa Miaka 50 Maisha yake. Mawakili wake wamesema alichapisha chapisho hilo katika Mechi ambayo Westbrom walipewa tano mtungi 5-0 na Manchester City katika uwanja Wa The Hawthorns. Silwood. Picha: jpeg.

Fury amshauri Bondia Anthony Joshua,kuelekea pambano la marudiano.

Picha
Nyota Wa pambano la dondi mshikilizi wa mkanda wa WBC Tyson Fury,amemshauri mpinzani wake mkuu Anthony Joshua AJ, anapojiandaa kumenyana na Oleksandr Usyk mwaka ujao. Utakuwa no mpambano Wa marejeano baada ya AJ kupokonywa mikanda yote na Usyk mbele ya mashabiki katika uwanja Wa Tottenham Hotspurs nchini uingereza mwezi septemba mwaka huu. "Ushauri wangu kwa Joshua katika pambano la marudiano,ni kupambana kwa nguvu, katika mbinu nzuri azijuazo,Anahitaji kuweka kiwango bora cha tabia na kufikiri kuhusu ushindi."Fury akizungumza na wanahabari. AJ na Fury kwenye pambano.

Ushauri Wa Engin Firat kwa FKF

Picha
SHIRIKISHO . Kocha mpya anayeifunza timu ya taifa la Kenya Harambee stars,Mturuki Engin Firat ,alilishauri shirikisho la kandanda nchini humo Fkf likiongozwa na Rais Nick Mwendwa,kuboresha Miundo mbinu kama vile ujenzi Wa viwanja na elimu kwa makocha. Engin wakati wake Wa kuzinduliwa rasmi,aliipa changamoto Fkf kwamba kama vijana wadogo hawatopata msingi sahihi,kutoka kwa makocha walioelimishwa ,basi itakuwa vigumu kuwafunza ukubwani. MAKOCHA. Kocha Firat ambaye anajiandaa kwa kibarua cha kuisaidia Stars kufuzu katika dimba la dunia Qatar 2022,aliwapa makocha nao changamoto ya kutotegemea kazi ya ukocha pekee kama kitega uchumi kwao. KANDARASI . Kuhusu kandarasi yake ya miezi miwili na stars,kocha huyu Wa zamani Wa Moldovia,alisema kuwa anataka kutathmini mazingira ya kazi kwanza na matokeo atakayotoa uwanjani.   kocha Firat na Rais Wa Fkf Nick mwendwa. Picha:Fkf media.

"Aondoke tu....." busquets asema

Picha
Kiungo Wa timu ya Barcelona Sergio Busquets amedamka kuwa "kitu rahisi kwa sasa ni kumpiga kalamu kocha", akizungumza baada ya mechi ya klabu bingwa barani uropa,wakizimwa na Benfica magoli matatu kwa karai.   Busquets akiwa uwanjani dhidi ya Benfica. MATOKEO MABOVU. Barcelona imekuwa na msururu Wa matokeo mabovu, akipiga sare dhidi ya Cadiz na Granada katika ligi kuu nchini Hispania Laliga,charazwa mechi mbili za klabu bingwa UCL ,ya kwanza akitiwa kambani na Bayern Munich  kamati ya nidhamu na hapo Jana kulabuliwa na Benfica 3-0, Darwin Nunez akifunga mawili na Rafa Silva moja.   Wachezaji Wa Benfica wakisherehekea ushindi dhidi ya Barcelona,goli la pili la Darwin Nunez. ..Getty images. KOCHA Hili la kocha ni mja dala mkubwa ila chini ya kocha Ronald koeman ,aliyewahi kuwa mchezaji Wa awali Wa wakali hawa Wa catalunya,Barcelona hawajapiga pasi hatarishi za kulenga lango kwa Mara ya pili kwenye mechi mbili mfululizo. Ronald koeman kwenye k

Ballon d'or kurejea mwezi Novemba

Picha
Tuzo la mchezaji bora Wa dunia kurejea mwaka huu baada ya kutupiliwa mbali mwaka uliopita kwa Mara ya kwanza tangu kuanza kwake miaka 64. Hafla hii imeratibiwa kufanyika tarehe 29 mwezi Novemba. Nyota Wa zamani Wa Chelsea na timu ya taifa Ivory Coast Didier Drogba na mwanahabari Wa michezo Sandy Heribert wanatarajiwa kuongoza sherehe hio. DROGBA NA SANDY.picha Hisani :Jpeg images. MSHINDI Tuzo la Balloon d'or kwa sasa mshikilizi ni nyota Wa kimataifa Wa Argentina Lionel Messi,akitarajiwa kuleta ushindani tena baada ya kuhamia Paris saint Germain ya ufaransa.Messi ameshinda Mara sita akifuatwa na Christiano Ronaldo Wa Manchester united. Lionel Messi katika hafla ya Balloon d'or. Picha Hisani: Getty images. USHINDANI .  Wengine waliorodheshwa katika kolamu ya ushindani mwaka huu ni mshambulizi Wa Bayern Munich Robert lewandwoski na kiungo kati Wa Chelsea Jorghino. Orodha rasmi kutolewa octoba 8.

Chelsea yazikwa,Ronaldo akiifufua United

Picha
Nyota Wa Manchester United Christian Ronaldo amefikisha magoli 136 katika michezo 178 ya michuano ya klabu bingwa bara uropa.Kwa sasa ni rekodi ya magoli mengi katika misimu 17 akiwa mchezaji Wa kwanza kufunga katika mechi 11 mfululizo.Ronaldo aliwapa united goli la  ushindi katika mechi dhidi ya villareal mtanange Wa klabu bingwa mwezi septemba tarehe 29 mwaka 2021. JUVENTUS DHIDI YA CHELSEA . Wakali Wa Turin Juventus maarufu Bikizee walimkwatua mwanadaraja Chelsea goli moja sifuri likifungwa na Federico Chiesa. Chelsea wameshindwa kufaidisha kutokuwepo kwa Morata Alvaro na Paul dyballa katika kikosi cha Juventus.  Matokeo katika mechi nyingine. picha Hisani: Jpeg na Being sports Author Paulo Mwanaspoti.

Juventus ni majeruhi kuelekea mpambano dhidi ya Chelsea.

Picha
Mfuma nyavu wa Uispania Alvaro Morata na Mwenzake Wa Argentina Paulo Dyballa, ni baadhi ya wachezaji muhimu ambao uenda wakakosa mechi dhidi ya Chelsea, usiku huu 29.9.2021 katika mkwaruzano Wa timu bora barani uropa. Kocha Massimiliano Allegro amedokeza kuwa uenda akalazimika kuwatumia Federico Chiesa na Moise Keane endapo atanyumbulisha mfumo Wa 3-5-2 na kuwatumia Leonardo Bonnuci na Dannilo kwenye viungo kati.Mechi ya mwisho Juventus kupatana Chelsea katika michuano hii Chelsea alimcharazwa magoli matatu kwa tairi.3-0.Wikendi iliyopita Juve maarufu bikizee alipata ushindi dhidi ya Malmo. CHELSEA . Upande wao wanachelsea naaangazia taarifa ya Tuchel Thomas, ambaye amesema ni vizuri kwa wachambuzi kudai kwamba ndio timu bora barani uropa kwa sasa. Hili linawaweka wapi kuelekea mpambano huu? Chelsea mechi ya wikendi walitunguliwa muhogo mmoja pakavu kwa maana ya goli moja sifuri. Picha hisani : Football daily.

"Wanalipwa 700 katika mechi za Harambee Stars...", Nyamweya atoa madai.

Picha
Taarifa ni changa mno kuhusu Nyota Wa kati Victor Mugubi Wanyama maarufu Simba Wa muthurwa kustaafu soka LA kimataifa.Ila kwa sasa wengi Wa wakenya wanajiuliza ni kwanini maana nafasi take kwenye kikosi cha taifa ipo wazi kama meno ya ngiri,kwa tajiriba yake akicheza zamani Celtic,Southampton na Tottenham Hotspurs. victor akiitumikia Spurs ya Uingereza.PICHA HISANI:JPEG. Kimetifuka baada ya aliyekuwa bosi Wa shirikisho la soka nchini Fkf Sam Nyamweya kusema kuwa,kiini cha wanyama kuacha stars ni Migogoro baina yake na viongozi Wa shirikisho kuhusu marupurupu katika mechi za dimba la Afcon Mwaka 2019,swala ambalo beki Abud Omar aliwahi kuligusia. Nyamweya akizungumza na waandishi habari Wa mtandao Wa Goal.com amekiri kuwa Wakati wake kila mchezaji wa anayecheza katika timu ya taifa alikuwa anapata 3,000 hadi 5,000 za kuingia kambini kwa siku ila sasa kulingana na wasosi wake Wa taarifa ,wanastars wanapokea 7,00 alizodai ni za watu Wa ujenzi maarufu mjengo.  Sam N

Isuza,Omalla na siraj kwenye kikosi cha wiki

Picha
Kinda Benson Omalla ,Whyvone Isuza Wa Bandari na siraj ni baadhi ya wachezaji waliojaaliwa kupata nafasi katika kikosi cha wiki ya kwanza,mitanange ya ligi kuu nchini Kenya Fkf pl iliyotimua vumbi. Omalla na Isuza wote walianza kwa kutikisa nyavu Mara mbili kila mmoja,Omalla akifunga dhidi ya Kcb na mwenzake akifunga dhidi ya slam boys Mathare united.Wengine waliojaaliwa kupata nafasi ni pamoja na Samuel Olwande wa kariobangi sharks na mlinzi wa wanajeshi Saruni.

MOH DEWJI AACHA UONGOZI SIMBA.

Picha
Pigo kwa mashabiki Wa Simba sc Tanzania baada ya Mwenyekiti Wa bodi ya wakurugenzi Mohammed Dewji kuacha wadhifa huo. Kwenye taarifa Moh amesema anasafiri sana kitu kinachomhangaisha sana katika usimamizi Wa klabu katika upeo huo. Mojawapo ya picha za Mohammed Dewji akiwa uwanjani katika mechi ya Simba. Picha hisani: Presenter page at Facebook. Moh amemteua naibu wake Salim Abdallah Muhene kuwa mwenyekiti Wa bodies hio.Muhene maarufu kama Try again amekuwa naibu Wa MOH kwa miaka minne. Abdallah Muhene. PICHA hisani: Michezo online Facebook.

"Nitampiga tena" Mwanadondi Usyk adamka.

Picha
Baada ya hivi majuzi mwanabondia maarufu Anthony Joshua AJ kupokonywa mikanda yote WBO,IBF na WBA na Mwenzake Wa Ukraine Oleksandor Usyk pambano lijalo lilikuwa la mkanda Wa WBC ambao una Tyson Furry,ila kwa sasa, baada ya AJ kuitisha pambano la marudiano sasa Usyk amesema yupo tayari. photo courtesy Ap. Oleksandor usyk Kikubwa katika pambano hili Usyk aliyeshinda mikanda yote katika uzani mwepesi sasa amedai kuwa atamchakaza tena AJ. Kwa sasa pande zote mbili hazijakubaliana kuhusu sehemu sahihi kwa pambano hili wakraine wakitaka lifanyike kwao na waingereza wakitaka lifanywe London.

ALIPATIKANA KITANDANI NA MKEWE

Picha
Kiungo kati Wa zamani Real Madrid Fernando Gago ametalikiana na mkewe baada ya kufumaniwa akiwa mtupu kitandani na mpango Wa pembeni. Kwa mujibu Wa taarifa zilizopeperushwa na Cynthia Fernandez Wa Argentine Tv,Mkewe Gago Gisela Dulko mwenye umri Wa 36 alimpata mumewe akila uroda na mwenye shule ya densi Veronica Lafitte na cha aibu zaidi katika kitanda chake. photo courtesy Ap.

DE BRUYNE ANAFAA NYEKUNDU.......

Picha
Mashabiki Wa Man united wamelalamikia viwango vya shirikisho la soka barani ulaya Uefa,kwa madai kwamba kiungo kati Wa Manchester city Kevin De Bruyne, alifaa kadi nyekundu kwa kumchezea ngware Kiungo Wa PSG Gana Queye. Kwa mujibu Wa washabiki Wa United kosa alilolifanya De Bruyne ndilo alilofanya beki wao Aaron wan Bissaka katika mechi dhidi ya Young Boys na kupigwa umeme kwa maana ya kadi nyekundu. Photos courtesy: Ap and Getty images.

"Tutakula na tulewe."Asema pep

Picha
Kocha Wa Manchester city pep Quardiola, akihojiwa baada ya mechi ya klabu bingwa barani uropa dhidi ya Mabosi Wa kiarabu PSG amesema kinachowasubiri baada ya kupewa kichapo cha mbili kavu uwanjani parc de princes, ni kula kunywa wine na kulala kusubiri mitanange ya wikendi.Magoli ya PSG yalifungwa na Idris Gueye na Mchawi Lionel Messi. MATOKEO KWENYE MECHI NYINGINE. Goli la pekee la Donny Malen liliwapa wajerumani Borrusia Dortmund ushindi Wa moja patupu. URENO. Ureno kulikuwa kubaya mno Liverpool ikiaribu hewa kwa kuichafua na mabomu matano kwa moja dhidi ya Porto. Kwenye matokeo mengine.

Quardiola kuhusu Messi,Neymar na Mbappe.

Picha
"Sijui nitawakaba vipi" .Kocha Wa Manchester city pep quardiola amesema hawajui ni namna gani ya kuwakaba mastaa watatu Wa PSG akijiandaa kumenyana nao katika uwanja Wa PARC de princes nchini ufaransa kwenye mechi ya klabu bingwa barani uropa.  watatu hawa hawajakuwa wakishiriki mechi nyingi pamoja ila Messi hapo Jana amerejea mazoezini. Kwa kocha pochettino ni kuchangua tu watakaoanza dhidi ya Manchester city.

Messi Tayari kuwavaa city

Picha
Nyota Wa dunia Lionel Messi amerejea mazoezini hili kuisaidia timu yake kujiandaa kumenyana na Manchester city katika mchezo Wa klabu bingwa barani Afrika katikati mwa Juma.

HAMILTON NDIYE BINGWA WA LANGALANGA

Picha
Mbio za magari ya langalanga mkondo Wa urussi zimekamilika, lewis Hamilton akitinga ushindi wake Wa 100. Hamilton hakutarajiwa kushinda na walevi wengi Wa mchezo huu baada ya mpinzani wake mkuu verstappen Max kuonyesha ushindani mkali katika raundi 20 za kwanza. Max's verstappen ameibuka Wa pili na kupokonywa ushindi huo ambao aliutwaa mapema mwaka katika Grand pix ya Uholanzi.

AFC leopards yayawashangaza mashabiki.

Picha
Wanachui AFC leopards wameduwaza mashabiki Wa ligi kuu nchini Kenya kwa kuichakaza Tusker united ambao ndio mabingwa Wa tetezi kichapo cha goli moja sifuri.

LIVERPOOL KILELENI

Picha
Liverpool inaongoza jedwali licha ya kuandikisha sare ya magoli matatu kwa matatu dhidi ya Brentford huku Mohammed Salah nyota kutoka taifa la  Misri akifikisha magoli mia moja mwenye ligi akiwa na wekundu Wa An field. Manchester city ni ya pili wakikazana alama na Chelsea na Manchester united wore alama 13.

YANGA BINGWA

Picha

Gor Mahia yaanza vizuri msimu mpya

Picha
Gor Mahia wameichakaza Kcb magoli mawili kwa moja yote yakitiwa kambani na Benson Omalla.Mmata Erick ameifungia kariobangi sharks goli la pekee dhidi ya posta  rangers.Malimbukeni wameandikisha sare kwa Vihiga Bullets kutoka sare tasa dhidi ya Bidco united na Talanta Fc wakiandika sare dhidi ya Wazito Fc ya kimanzi. Sajili mpya upande wa Bandari Wyhvone isuza amekuwa na siku nzuri akitingisha kamba mara mbili na kuisaidia Bandari kuvuna ushindi wa magoli matatu kwa sifuri iliyomilikiwa na Mathare United.

LIGI KUU NCHINI KENYA YAREJEA.

Picha
Fkfpl yarejea bila mdhamini.Ligi hii inaandaliwa wakati huu wadhamini walioekeza kiasi kikubwa cha fedha kama vile kampuni za mchezo wa kamari Betking na odibets wakijiondoa.Wadhamini wengine waliosalia ni pamoja na kituo cha kupeperusha matangazo Milele FM na Televisheni ya Star times.Je, vilabu    vilivyo na ukata Wa fedha zifanyeje?