Mshambulizi pekee anayemvuruga Virgil Van Dijk
VIRGIL KWA ERLING HAALAND.
Beki kati Wa Liverpool na taifa la Uholanzi, Virgil Van dijk amemsifia mshambuliaji wa Borussia Dortmund Erling Haaland, kwa kusema Ni moja ya mastaa Wa sasa walio na kila kiungo kumbabaisha beki mzuri duniani.
"Haaland ni straika wa kipekee kwani ana nguvu,ana mbio na kila kiungo cha kumsababishia beki maisha magumu," Virgil akizungumza na Sky sports.
Mwamba huyu Wa Netherlands ameongeza kwamba ,muundo wake Wa kucheza Ni kama ule Wa James Jamie Vardy Wa Uingereza na Leicester. "Ana nguvu zaidi ya vardy ila mchezo wao Ni mmoja" dijk akaongeza.
PICHA:GETTY IMAGES.
KUTUA ANFIELD.
Mshambulizi huyu amehusishwa pakubwa na wekundu Wa An field akitajwa kama mrithi Wa Takumi minamino na Firmino ambao kiwango chao sio cha magoli kila Mara.
Baada ya Virgil kumtilia shombo nyota huyu akisema Ni moja kati ya washambulizi walionitatiza,uenda hili likapandisha homa ya Liverpool kumnyakua katika dirisha la uhamisho lijalo. Dau lake sokoni Ni £68million.
Mwandishi
Mwanamichezoo blog
E-mail: Michezoh@gmail.com
Maoni
Chapisha Maoni